Ushirika wa Mradi wa Pamoja wa Korosho (KCJE Ltd) una jukumu muhimu la kuhakikisha wakulima wanapata pembejeo na viuatilifu bora kwa ajili ya uzalishaji wa korosho kwa wakati muafaka.





Katika kujiandaa na msimu mpya wa korosho wa mwaka 2026/2027, ushirika unaendelea na maandalizi mbalimbali ya kuhakikisha pembejeo pamoja na viuatilifu vinapatikana kwa wingi na kwa wakati ili kuwasaidia wakulima kuongeza tija na ubora wa mazao yao.





Hatua hizi ni sehemu ya juhudi za KCJE Ltd katika kuimarisha uzalishaji wa korosho, kuongeza kipato cha wakulima, na kuchangia maendeleo ya sekta ya korosho nchini. Ushirika utaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha wakulima wanapata huduma bora zinazowezesha uzalishaji wenye tija na endelevu.












